HALMASHAURI YA USHETU WAADHIMISHA SIKU YA UPANDAJI MITI LEO WILAYANI KAHAMA

MTAALAMU YA UPANDAJI MITI KUTOKA  TUMBAKU AKITOA MAELEKEZO JINSI YA KUPANDA MITI HIYO HUKO KIJIJI CHA KANGEME KATA YA ULOWA WILAYA YA KAHAMA.

Upande wake kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ushetu Anna Ngongi amesema uchumi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu unategemea zao la tumbaku hivyo haiwezekani kukata miti tu bila kupanda mingine ambayo itaendelea kutumika hapo baadae.
Ngongi ameeleza kuwa  zao la tumbaku linahitaji sana miti,hivyo wananchi na hasa wakulima wawe chachu ya kuhamasisha maendeleo kwa kupanda miti mingi katika maeneo yao ambapo wao ni watumiaji wakubwa.
Aidha aliwashukuru wadau walioshiriki zoezi hilo la upandaji wa miti hususani kampuni ya Tumbaku ATTT kwa kutoa elimu ya Ugani na hifadhi ya mazingira pamoja na bodi ya Tumbaku kwa kuratibu maendeleo ya zao hilo wilayani. 
Maadhimisho haya hayo ya upandaji miti katika halmashauri ya Ushetu hufanyika disemba mbili kila mwaka ambapo katika msimu wa mwaka 2014/2015 imepanga kupanda miti ipatayo 2,726,438 huku kauli mbiu ikisema “Panda Miti ikutunze”.

MTENDAJI WA KATA YA ULOWA AKIMKARIBISHA MGENI RASMI NA WAGENI KUTOKA WILAYANI KWA AJILI YA ZOEZI LA KUPANDA MITI ,ALIYEVAA TRAKISUTI  KATIKATI NI KAIMU MKURUGENZI WA HALAMASHAURI YA USHETU BI ANNA NGONGI NA WATUMISHI WENGINE WA HALMASHAURI HIYO.
PICHA ZAIDI

KAIMU MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA USHETU MH TABU KATOTO AKIONGEA KATIKA ZOEZI HILO.
BWANA TITO MWELE MKULIMA ALIYETOA SHAMBA LAKE KUPANDA MITI KAMA MKULIMA WA MFANO.


ZOEZI LA UPANDAJI LILIPAMBA MOTO LICHA YA MVUA KUBWA KUNYESHA WAKATI WATUMISHI NA WADAU WAKIENDELEA KUPANDA MITI.

WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI KANGEME PIA HAWAKUWA NYUMA KATIKA KUPANDA MITI.




WADAU WAKIENDELEA KUPANDA MITI.

WADAU TOKA KAMPUNI YA TUMBAKU ATTT PIA WALIKUWEPO KATIKA KUPANDA MITI.




0 comments: