WATU ZAIDI YA 200 WANUSURIKA KUFA BAADA YA NDEGE WALIYOKUWA WAMEPANDA KULAZIMIKA KUTUA KWA DHARURA KATIKA KIWANJA KIDOGO ARUSHA ...!!
Abiria zidi ya 200
waliokuwa wamepanda ndege aina ya 5H ET-AQW mali ya Shirika la ndege la
Ethiopia iliyokuwa ikitoka nchini Ethiopia Kwenda katika uwanja wa ndege
wa Kimataifa mkoani Kilimanjaro (KIA) wamenusurika kufa baada ya Uwanja
wa kia kuwa na hitilafu hivyo kulazimika kutua katika kiwanja Kidogo
cha Kisongo jijini Arusha.
Kwa mujibu wa Taarifa zilizotufikia
ndege hiyo imelazimika kutua katika uwanja mdogo wa ndege wa Kosongo
ulioko Jijini Arusha, na kuzua hofu kwa watu wa eneo hilo.
![]() |
| Ndege hiyo ikiwa uwanjani hapo huku tairi la mbele likiwa limezama kwenye udongo pembeni kutokana na uwanja huo kuwa mdogo |
Hadi sasa shughuli za uokoaji zilikuwa
zikiendelea, Taarifa kuwa ni hitilafu gani iliyotokea bado hatujaipata,
na pindi tutakapoipata tutakufahamisha.
![]() |
| Jinsi Ndege hiyo ilivyoacha uwanja na kuingia kwenye ukoka |
![]() |
| Wananchi wa jiji la Arusha Wakiangalio tukio hilo kubwa kwao |
![]() |
| Kama inavyoonekana katika picha kikosi cha Zimamoto nacho hakikuwa nyuma |
![]() |
| Wananchi wakiwa wamekaa kuangalia hali ilivyo |
![]() |
| Baadhi ya watu na viongozi mbalimbali waliokuja na magari kuangalia tukio hilo |
![]() |
| Kweli hali ilikuwa tete |
![]() |
| Uwanja ulivyo mdogo na Ukubwa wa ndege iliyotua |
![]() |
| Magari ya zimamoto yanazidi kuongezeka |
![]() |
| Baadhi ya wananchi wakijaribu kufahamisha jamaa zao juu ya tukio hilo japo kwa simu |
![]() |
| Hali ya jiji la Arusha ilivyo ya Baridi na Ukungu kwa siku ya leo |
Kwa hisani ya Emmanuel Mlelekwa - Arusha.












0 comments: