Jenerali Honore Traore mkuu wa jeshi la Burkina Faso aliyejitangaza rais mpya wa nchi hiyo Mkuu
wa Jeshi la Burkina Faso Jenerali Honore Traore sasa amejitangaza kuwa
rais baada ya aliyekuwa rais wa Burkina Faso Blaise Compaore kutangaza
kujiuzulu. Jenerali Traore ameshinikizwa na waandamanaji ambao walikuwa wanamtaka kuchukua usukani baada ya kuondoka kwa Bwana Compaore. Bwana
Compaore amesema kuwa amekubali kuondoka madarakani ili kutii matakwa
ya waandamanaji ambao hawamtaki kuendelea kuongoza taifa hilo hata baada
ya kutawala kwa miaka 27. Bwana Compaore sasa ametaka uchaguzi mpya wa urais ufanyike baada ya siku 90. Awali msemaji wa jeshi alikuwa amewaambia waandamanaji kuwa bwana Compaore hayuko tena madarakani huko Ouagadougou. Maelfu ya waandamanji walikuwa wamerejea mabarabarani kwa siku ya pili Hata hivyo hakubaini ikiwa afisa huyo wa kijeshi alikuwa akizungumza kwa niaba ya jeshi lote. Jeshi lilisema kuwa litafanya mkutano na waandishi habari. Siku
ya Alhamisi waandamanaji waliokuwa wamekasirishwa na jitihada za rais
za kuongeza muda wa uongozi wake baada ya kutawala kwa miaka 27
waliteketeza jengo la bunge na kuvamia kituo cha televisheni ya taifa. Bwana
Compaore alitupilia mbali jitihada za kubadilisha katiba ambayo
ingemruhusu kuwania tena muhula mwingine kama rais lakini akasema kuwa
angebaki madarakani kwa mwaka moja zaidi.via>>BBC |
0 comments: