MAMA AJIFUNGUA MTOTO WA AJABU HUKO DAR.
Na Dustan Shekidele, Morogoro
My God! Mama aliyetambulika kwa jina la Swaumu
Sadick (25), mkazi wa Manzese jijini Dar, amejikuta yeye na manesi
wakitimua mbio kwa woga baada ya kujifungua kiumbe wa ajabu.
Swaumu Sadick akiwa hospitali baada ya kujifungua mtoto huyo.
Kwa mujibu wa shuhuda wetu, tukio hilo ambalo kwa sasa ni gumzo,
lilijiri hivi karibuni mishale ya saa 8:00 usiku kwenye Kituo cha Afya
Cha Kijiji cha Mlali kilichopo wilayani Mvomero mkoani hapa.
Katika tukio hilo, ilielezwa kwamba Swaumu alijifungua kiumbe huyo wa ajabu anayedaiwa kuwa na mkia mrefu huku akiwa hana miguu.
Katika tukio hilo, ilielezwa kwamba Swaumu alijifungua kiumbe huyo wa ajabu anayedaiwa kuwa na mkia mrefu huku akiwa hana miguu.
Ilidaiwa kwamba baada ya kutokea kwa tukio hilo, baadhi ya ndugu
walishikwa na taharuki kubwa huku wengine wakitoa taarifa kwa
mwanahabari wetu ambaye alifunga safari kutoka mjini Morogoro na
kuwasili kwenye kituo hicho cha afya majira ya saa 12:00 asubuhi.
Katika mahojiano maalum na gazeti hili juu ya tukio hilo, nesi wa
zamu aliyekutwa kituoni hapo aliyejitambulisha kwa jina moja la
Consolatha alikuwa na haya ya kusema: “Nilimpokea Swaumu majira ya saa
1:00 usiku akilalamika kuwa na uchungu wa kujifungua.
Swaumu Sadick akiuguzwa hospitali.
“Nilimpa kitanda. Saa 8:00 usiku, uchungu ulizidi nikampeleka leba
ambako alijifungua kiumbe huyo mwenye jinsi ya kiume. “Baada ya
kujifungua na kumuona kiumbe huyu wa ajabu, nilitimua mbio usiku huo kwa
woga na kwenda kuamsha manesi wenzangu wanoishi kota za kituo hiki cha
afya.
“Nimefanya kazi hii ya ukunga na kuzalisha wazazi zaidi ya 50 lakini sijawahi kukutana na tukio kama hili.”
Kwa upande wake mganga mkuu wa kituo hicho aliyejitambulisha kwa jina moja la Dk. Beatrice alikuwa na haya ya kusema juu ya tukio hilo la kusikitisha:
Kwa upande wake mganga mkuu wa kituo hicho aliyejitambulisha kwa jina moja la Dk. Beatrice alikuwa na haya ya kusema juu ya tukio hilo la kusikitisha:
“Kimsingi si kiumbe ila ni mtoto ambaye awali tulipomcheki mzazi
tulibaini ana kichwa kikubwa na alishafia tumboni zaidi ya siku tatu.
“Amezaliwa akiwa na miezi nane tumboni. Tulichokifanya ni kuokoa maisha ya mama jambo ambalo tumefanikiwa.”
“Amezaliwa akiwa na miezi nane tumboni. Tulichokifanya ni kuokoa maisha ya mama jambo ambalo tumefanikiwa.”
Mtoto wa ajabu aliyezaliwa na Swaumu.
Akizungumza kwa tabu na mwanahabari wetu, Swaumu alisema: “Hii ni
mimba yangu ya tatu, ya kwanza iliharibika tumboni, ya pili nilifanikiwa
kuzaa salama mwanangu Maimuna.
“Hii ya tatu ndiyo nimejifungua kitu hiki cha ajabu.”
“Hii ya tatu ndiyo nimejifungua kitu hiki cha ajabu.”
Alipoulizwa kwa nini aliondoka Dar ambako ndiko kwenye hospitali
kubwa na kwenda kujifungulia kijiji akijua ana matatizo ya uzazi, mama
huyo alisema:
“Siku za kujifungua zilipokaribia mume wangu Abdallah aliniambia nije kujifungulia kwa bibi yangu Halima, kwa bahati mbaya ndiyo yametokea haya.”
“Siku za kujifungua zilipokaribia mume wangu Abdallah aliniambia nije kujifungulia kwa bibi yangu Halima, kwa bahati mbaya ndiyo yametokea haya.”
Kwa upande wake shangazi wa Swaumu aliyekutwa akimhudumia alisema:
“Yameshatokea ya kutokea, tunamshukuru Mungu na tunajiandaa kumchukua
mjukuu wetu tukamzike.”
0 comments: