MSANII AFA AKITAJA JINA MAINDA
Stori: Imelda Mtema MSANII
aliyefariki dunia hivi karibuni mjini Morogoro, Sherry Magali, anadaiwa
kuwa alikuwa akilitaja jina la Ruth Suka ‘Mainda’ kila mara hadi
alipofikwa na umauti.
Marehemu Sherry Magali enzi za uhai wake.
Chanzo chetu makini kilichokuwa karibu na
msanii huyo wa filamu, kinasema Sherry alianza kugoma kula akidai hadi
amuone msanii mwenzake huyo ambaye alikuwa jijini Dar es Salaam
anakoishi.
Msanii wa 'Bongo Movie' Ruth Suka (Mainda) akiwa katika pozi.
Mpashaji huyo alisema hata siku aliyofariki
pia alilitaja jina hilo, kitendo kilichowaumiza sana baadhi ya ndugu na
marafiki. Mainda ambaye alikuwa ni rafiki wa marehemu, alikiri kusikia
jambo hilo na anasikitika kwamba siku aliyopanga kwenda, ndiyo ambayo
mwenzake alifariki.
0 comments: