UMESIKIA HII:MKE WA AFISA WA POLISI ALIVYOFUMANIWA NA MCHUNGAJI



Habari kubwa iliyoenea kwenye mitandao ambayo huenda hujabahatika kukutana nayo tarehe 4 november ni kuhusiana na fumanizi lililofanywa na askari polisi katika gari ambapo watu wawili wamekutwa wakifanya mapenzi mchana wa jua kali. 
 
Mitandao ya Zimbabwe imeandika kuhusiana na mchungaji Novert Chivese kukutwa akifanya mapenzi na mke wa afisa wa polisi msituni.
 
Habari  zinaarifu  kuwa baada ya wawili hao kukutana waliondoka ndani ya gari na kulekea kwenye msitu huo na kuendelea na kitendo hicho ambapo askari polisi waliofika eneo hilo walishtushwa baada ya kuona gari inatikisika kwa nguvu, baada ya kusogea karibu ndipo wakabaini kinachoendelea baina ya wawili hao.
 
Mwanamke huyo Fortunate Safuri ameolewa na Allen Tafirei ambaye ni askari wa idara ya Polisi ya Beatrice, Zimbabwe ambapo wana zaidi ya miaka nane kwenye ndoa yao.
 
Baada ya kuwafuma waliwapeleka kituo cha Polisi na kupigwa faini ya kiasi cha dola 20 kila mmoja kwa kosa la kufanya mapenzi hadharani, japo hatma ya ndoa zao bado haijafahamika.

0 comments: