AJALI YA GARI YAJERUHI 17 WILAYANI KAHAMA


Watu 17 wamejeruhiwa baada ya gari la abiria walilokuwa wakisafiria kutoka ulowa kwenda mjini kahama kuacha njia na kupinduka katika kijiji cha Nyandekwa wilaya ya kahama mkoani Shinyanga.
 
    
Ajali hiyo imetokea leo asubuhi ikilihusisha gari namba T 208 AGE lilokuwa likiendeshwa na dereva aliyetajwa kwa jina la Rashid Ramadhan mkazi wa Kahama mjini, ambaye hata hivyo alitoroka baada ya tukio hilo.
Kwa mujibu wa daktari mfawidhi wa hospital ya wialaya ya Kahama, Deogratius Nyaga, jumla ya majeruhi 5 wamepatiwa matibabu na kuruhusiwa huku 12 wakiwa wanaendelea na matibabu hospitalini hapo.
                                       
Mgonjwa akiwa amepumzika baada ya kupatiwa huduma

Daktari mfawidhi wa hospital ya wialaya ya Kahama, Deogratius Nyaga akiongea na waandishi wa habari
Daktari Nyaga amewataja waliolazwa kuwa ni Elizabert Mgesa (49), Katarina Makoye (32), Eliza Timotheo (30), Ngeke Chanila (23), Zawadi Andrea (18), Amos Hussein (32) na Adam John (20) ambaye alikuwa kondakta wa gari hilo. 
Wengine ni Zakaria Leonce (25), Mabala Paulo (28), Hamis Makala (26), John Marcel (26) na Michael Rashid (47) na motto benad Paulo mwenye umri wa miezi mitano na kwamba wote hali zao zinaendelea vizuri.
Jeshi la Polisi wilayani kahama limethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kwamba uchunguzi wakubaini chanzo chake unafanywa, huku juhudi za kumtafuta dereva wa gari hilo zikiendelea.
 
 
 
HABARI KATIKA PICHA
Majeruhi akiwa na ndugu yake ambaye amekwenda kumtembelea

Askari polisi akiwa akichukua maelezo kwa majeruhi kwenye wodi ya wanaume

Askari wa usalama barabarani akichukua amelezo kwa majeruhi kwenye wodi ya wanawake
Ajabu sana: Majeruhi wawili wakiwa katika kitanda kimoja
Mama aliyejeruhiwa pia katika ajali hiyo

Majeruhi wa ajlai hiyo wakiendelea kupata matibabu katika Hospitali ya Wilaya.

Hawa ni majeruhi walioshare kitanda kutokan ana uhaba wa vitanda,je hali ya maambukizi inadhibitiwa vipi ikiwa wote wamejeruhiwa na wanalala kitanda kimoja? 


0 comments: