SERIKALI IMEAHIDI KUDHIBITI UKATILI UNAOFANYWA DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO...!!
Serikali imesema itaendelea
kutekeleza sera na mipango ya nchi ili
kuhakikisha vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto vinakomeshwa na
hatimaye kujenga jamii yenye amani na furaha.
![]() |
| Naibu waziri wamaendeleo ya jamii, jinsia na watoto Ummy Mwalimu akihutubia katika sherehe za maadhimisho hayo. |
Hayo yamesemwa leo na naibu
waziri wa maendeleo ya jamii, jinsia na watoto Ummy Mwalimu, katika kilele cha maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa
kijinsia yaliyofanyika katika kata ya bugarama wilaya kahama mkoani Shinyanga.
Mwalimu amesema Tanzania
bado inakabiliwa na changamoto ya ukatili wa kijnsia ambapo takwimu zinaonyeha
kati ya wanawake 100 wenye umri kati ya miaka 15-49, asilimia 39 ya wanawake
hao hufanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Aidha amesema katika takwimu
zilizofanywa na wizara hiyo kwa kushirikiana na shirika la UNICEF zimeonyesha
kuwa watoto watatu kati ya watoto 10 hufanyiwa vitendo vya ukatili wa kingono.
Amesema vitendo hivyo
vimekuwa vikifanyika katika maeneo ambayo mtoto anajua ni maeneo salama ambayo
ni majumbani, mashuleni na katika jamii ambayo imekuwa haiko tayari kutoa
taarifa katika vyombo vya dola akitolea mfano dawati la jinsia, polisi na TAKUKURU.
Hata hivyo Mwalimu ameitaka
jamii kutoa taarifa kwa kupiga simu ya bure katika namba 116 ili kutoa taarifa
za unyanyasaji wa kijinsia na kukomesha tatizo la ukatili wa kijinsia katika
jamii.
![]() |
| Naibu waziri akifungua mziki katika maadhimisho |
![]() | |
| Wanafunzi wa shule mablimbalia walikuwepo pia katika mahadhimisho hayo ambapo pia ni wahanga wakubwa wa vitendo vya ukatili. |










0 comments: