BREEEEEAKING NEWSSS>> RAIS KIKWETE AWAFUTA KAZI MAWAZIRI WANNE



Rais Jakaya Kikwete ametengua uteuzi wa mawaziri wanne kufuatia ripoti ya kamati ya bunge kuhusu operesheni tokomeza kubaini uzembe wa vyombo wanavyosimamia. 
Akitoa taarifa hiyo bungeni waziri mkuu Mh. Mizengo Pinda amesema mawaziri hao wanne ni waziri wa maliasili na utalii balozi Hamis Kagasheki, waziri wa mambo ya ndani Dr. Emmanuel Nchimbi na waziri wa ulinzi Mh. Shamsi Vuai Nahodha na Dr. Mathayo David Mathayo wa mifugo, na maendeleo ya uvuvi.

                                          
                                                    Waziri Mkuu Mizengo Pinda.


 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Khamisi Kagasheki.

 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi.

 
                         Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha. 
Waziri wa Mifugo Mathayo David
 Mawaziri hao wamevuliwa uongozi baada ya Taarifa ya Kamati ya mali asili na Mazingira chini ya mwenyekiti wake James Lembeli kubaini unyama uliofanywa katika Operesheni Tokomeza majangili ambayo wizara za mawaziri hao wote zimehusika.
Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi mali asili na Mazingira James Lembeli




Source-Dunia Kiganjani

0 comments: