MISS SHINYANGA KUFANYIKA JUNE 28 NDANI YA UKUMBI WA NSSF MJINI KAHAMA.
Wanyange wakiwa wamavalia mavazi ya mdhamini wa soda ya coka cola katika mashindano makubwa ya miss shinyanga 2014
JUMLA ya Wanyange 20 Wanatarajia kushiriki katika
kinyang’anyiro cha kumpata mrembo wa Mkoa wa Shinyanga yatakayofanyika katika
ukumbi wa NSSF Wilayani Kahama.
Mashindano hayo yanayoratibiwa na Kampuni ya Asela
Promotion ya Mjini Kahama yatawashirikisha jumla ya warembo 20 kutoka katika
Wilaya sita za Mkoa wa Shinyanga ambazo ni Kishapu, Kahama, Shinyanga Mjini,
Msalala Shinyanga Vijijini na Ushetu.
Mratibu wa Mashindano hayo Asela Magaka alisema kuwa
mashindano ya kumtafuta mrembo wa Mkoa wa Shinyanga yanatarajiwa kuwa na mvuto
mkubwa kwa mashabiki kutoka na warembo hao kuwa na viwango vinavyofafa hali
ambayo italeta ushindani mkubwa miongoni mwao.
Magaka alisema kuwa mashindano hayo yanatarajia
kufanyika tarehe 28/6/2014 katika ukumbwa Kisasa maarufu na mpya wa Shirika la
hifadhi ya jamii (NSSF) Mjini Kahama na kuwataka mashabiki na wapenzi
kujitokeza kwa wingi katika kushudia nani anatwaa taji laMrembo wa Mkoa wa
Shinyanga.
Mratibu huyo alisema kuwa katika shindano hilo
linatarajiwa kupambwa na Wasanii kutoka ndani na nje ya nchi wakiongozwa na
mfalme wa Taarabu Nchini Mzee Yusuph, Amani kutoka Kenya na Mo Music.
Shindani hilo pia linatajiwa kudhaminiwa na
wadhamini mbalimbali wakiwemo SSCN TV ya Mjini Kahama, Nonema Investiment,
Trixie Social Media Market, Nyamizi Secretarial Service, Royal Supermarket,
NSSF, Coca Cola, Redds Global Publisher.
Wengine ni pamoja na Kijukuu Blog,Clouds FM, Three Jays’s
Inverstment, CXC Africa, Williamson Diamond, Salut, Ihesa Hotel, Kahama
Commonity Health Dispensary, Tulliz Fashion, Ngeleja Gold Mine, Kahama Motel,
Charitk Pub, Glory Pub na Barrick Buzwagi.
Mratibu huyo pia alisema kiingilio katika shindano
hilo kinatarajiwa kuwa shilingi 60,000 kwa watu wa jukwaa maalumu ( VIP) wakati
shilingi 20,000 kitakuwa ni kwa watu wa jukwaa la kawaida.
MATUKIO KATIKA PICHA:
muandaji wa mashindano ya urembo mkoa wa shinyanga Asela Magaka akiongea na warembo ambao hawapo pichani
wadhami wa shindano ya miss shinyanga salome makamba na mdhamini mkuu redds vegula
Afisa utamanduni wa wilaya ya kahama
julias kambarange wa upande wa kulia akiwa na muandaji wa mashindano
hayo asela magaka wakati wa utabulisho wa wadhami katika ukumbi wa hotel
ya ihesa hotel mjini kahama
wadhamini wa wanyange wa shindano la miss shinyanga wake pamoja na mdhami wa hotel ya ihesa ismail lunge
miongoni mwa mdhami wa shindano hilo
toka mgodi wa dhahabu wa buzwagi salome makamba mwenye kofia nyeusi
.kati ni mdhamini mkuu wa mashindano hayo toka kampuni ya tbl vegula
wanyange wanao wania taji miss shinyanga 2014
Muandaji wa mashindano ya miss
shinyanga Asela magaka akiongea jambo na afisa utamaduni wa wilaya ya
kahama julias kambarange kwenye utambulisho wa waadhami wa mashinda hayo
Baadhi wa wadhami wa mashindano ya unyange mkoa wa shinyanga wakiwa katika utabulisho
Mwenye kofia nyeusi moja wa wadhamini
wa kampuni ya soda ya coka cola bwana chacha wakati wa kutambulisha
katika udhami wa miss shinyanga
Baadhi ya wadhamini wa miss shinyanga wakiteta jambo
Moja wa wadhamin wa mashindano ya miss shinyanga patrick james mwenye kofia nyeusi
MDHAMINI MKUBWA MISS SHINYANGA KINYWAJI CHA REDDS VIKIWA KATIKA MAADALIZI YA MUONEKANO WAKE
Moja wa wadhami wa miss shinyanga
patrick james mwenye kofia nyeusi wakitafakali juu ya shindano la miss
shinyanga ambalo linatarajiwa kufanyika katika ukumbi wa Nssf wilayani
kahama tarehe 28,6,2014
Wanyange wa miss shinyanga wakiwa katika moja ya mazoezi yao katika ukumbi wa ihesa hotel mjini kahama
Muandaji wa miss shinyanga Asela magaka akiongea na wadhamini wa miss shinyanga katika hotel ya ihesa mjini kahama
Baadhi ya wangeni walioambatana na wadhami wa miss shinyanga 2014 mjini kahama
washiriki
wa unyange mkoani shinyanga wakimsikiliza wadhamini wa miss shinyanga
2014 mjini kahama ambapo mashindano hayo yatafanyika wilayani hapa.
0 comments: