MAIGE AELEZEA MGOGORO WA WANANCHI WAKE KUHUSU MAKAO MAKUU YA JIMBO LA MSALALA.



Hatimaye mbunge wa jimbo la Msalala wilayani kahama Ezekieli Maige ametoa ufafanuzi juu ya mgogoro wa wananchi wa jimbo lake wanaogombea kujengwa eneo la Makao makuu ya halmashauri mpya ya msalala
 
Akiongea kwa njia ya simu kutoka Dodoma jana Maige ambaye amewahi kuwa waziri wa Maliasili na utalii amesema suala hilo  ni la kiutendaji na si la kisiasa kama baadhi yao wanavyotaka kulipeleka
 
Katika halmashauri ya Msalala iliyogawanywa kutoka wilaya ya Kahama Madiwani wake wanamvutano mkubwa wa eneo la kujenga makao makuu  ya  halmashauri hiyo ambapo wengine wanadai yajengwe kata ya Segese na baadhi yao wanadai kujengwa kata ya Busangi
 
Kufuatia hali hiyo Maige amewataka wananchi hao watambue kuwa maombi yao hakuna mwenye asilimia mia moja ya kukubaliwa isipokuwa maombi yote ya Segese na Busangi yapo kwa asilimia hamsini kila mmoja
 
Kauli hiyo ilikuja baadhi  ya  wananchi hao kumtuhumu kuwa amekwamisha makao hayo kujengwa Segese hali ambayo Maige amesema yeye kama Mbunge  hana mamlaka ya kugawa makao makuu ya halmashauri na kuongeza kuwa kwake wananchi wote wa Segese na Busangi ni sawa
 
Aliwataka wananchi hao waelewe kuwa madiwani wao ndio waliopendekeza makao hayo kwa muhutasari ya vikao halali ukiwemo uliopendekeza kujengwa Busangi na ule wa kubadilisha kupeleka Segese hivyo ni uamuzi wa waziri mkuu kumaliza tatizo hilo na si mbunge kama wanavyodai

0 comments: