MADREVA WANAOEGESHA MAGARI VIWANJA VYA CDT. WAWATUHUMU ASKARI WA DORIA KAHAMA KUOMBA RUSHWA KWAO
.

PICHA HII HAISADIFU UHALISIA (KUTOKA MAKTABA)
Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga
linafuatilia uchungunzi wa askali polisi wa doria wilayani Kahama ambao
wanatuhumiwa kuwanyanyasa wamiliki wa magari ya mizigo ambao huegesha kwenye
eneo la halmashauri ya mji la CDT
Kauli hiyo imetolewa leo na kamanda
wa polisi mkoa wa Shinyanga Jastus Kamugisha wakati akiongea na RFA baada
ya kutakiwa kuzungumzia malalamiko hayo yaliyotolewa kwa wandishi wa habari na
wamiliki wa magari hayo
Katika malalamiko hayo wamiliki hao
wamedai askali wa doria badala ya kwenda kusaka waharifu wamekuwa wakiishia
kwenye maegesho ya CDT ambapo hutumia vitisho mbalimbali kwa kuwakamata madreva
wanaoshindwa kuwapa rushwa kati ya shilingi laki moja hadi laki tatu
Hata hivyo mwenyekiti wa halmashauri
ya mji wa Kahama Machibya Shidulamabambasi inayomiliki eneo hilo la
maegesho ya CDT amesema tuhuma za madai hayo atazifikisha kwa mkuu wa wilaya ya
Kahama kwa kuwa ndiyo mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya
Kufuatia hali
hiyo kamanda Kamugisha amesema jeshi lake litahakikisha linafuatilia tuhuma
hizo na watakao bainika watachukuliwa hatua za kinidhamu kwa kufuata taratibu
za kipolisi kwa kuwa kazi ya polisi ni kulinda raia wema na mali zao.
Credit:Shija Felician.
0 comments: