CCM WAIBUKA KIDEDEA KATIKA UCHAGUZI WA WENYEVITI NA MAKAMU WILAYA YA MBOGWE NA BUKOMBE
| MKUU WA MKOA WA GEITA MAGALULA SAID MAGALULA AKIWA NA VIONGOZI MBALIMBALI WA WILAYA YA BUKOMBE NA MBOGWE KATIKA KIKAO CHA KUVUNJA BARAZA LA MADIWANI NA KUCHAGUA MWENYEVITI NA MAKAMU WAO. |
Viongozi
wa halmashauri ya wilaya za mbogwe na bukombe mkoani geita wametakiwa kufanya
kazi kwa ushirikiano na kufuata kanuni za uongozi wa umma ili kuepuka migogoro
katika halmashauri hiyo.
Hayo
yamesemwa leo na mkuu wa mkoa wa geita magalula said magalula katika kikao cha
kuvunja baraza la madiwani na kuchagua viongozi wapya kilichofanyika katika
ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya bukombe.
Magalula
amesema viongozi watakaochanguliwa wanapaswa kuwa mfano wa kuigwa na hivyo
watumie vizuri nafasi zao ili kuleta maendeleo katika wilaya zao.
Katika
kikao hicho ambacho kilikuwa cha kuvunja baraza la madiwani na kuchagua uongozi
mpya mkurugenzi wa halmashauri ya bukombe lilian matinga amemtangaza mwenyekiti
wa kuwa ni joseph kurya ccm aliyepata kura 12 kati ya kura 19.
Nafasi
ya makamu mwenyekiti imechukuliwa na
lameck warangi kwa tiketi ya ccm
aliyepata kura 14 dhidi ya mpinzani wake yusuph fungameza aliyepata kura 5 kati
ya kura 19.
Hata
hivyo mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya mbogwe Sophia kumbuli amemtangaza
mwenyekiti wa wa halmashauri hiyo vicent busiga na makamu wake nsika sizya
waliopita bila vikwazo kutokana na
kutokuwa na wapinzani.
MATUKIO KATIKA PICHA.
| MKUU WA MOA WA GEITA AKIZUNGUMZA KATIKA KIKAO CHA KUVUNJA BARAZA LA MADIWANI BUKOMBE NA MBOGWE PEMBENI KULIA KWAKE NI MKURUGENZIWA BUKOMBE LILIAN MATINGA NA DC WA MBOGWE KUSHOTO KWAKE HUSNA MWILIMA. |
0 comments: