Kampuni ya utafiti Resolute imekabidhi madawati 31 kwa shule ya msingi Kanegele.

MENEJA WA KAMPUNI YA RESOLUTE WILLIAM HARMWORTH AKIJADILIANA JAMBO NA MKUU WA WILAYA MEJA MSTAAFU BAHATI MATALA KABLA YA KUKABIDHI MADAWATI SHULE YA MSINGI KANEGELE.

AKIKABIDHI MADAWATI KWA DIWANI WA KATA YA BUKANDWE LUTENI MSTAAFU HENLYMALISHI




MWALIMU MKUU AKIKABIDHIWA MADAWATI NA M/KITI WA

MWANDISHI NA MMILIKI WA BLOG HII HERIETH KATIKIROAKICHUKUA PICHA KWA AJILI YA BLOG

JONES NYAKWANA MJEOLOGIA KUTOKA RESOLUTE

HERIETH AKIWA NA WALIMU WA SHULE YA MSINGI KANEGELE
      

RESOLUTE WATUMIA MILIONI 47.7 KWA JAMII KATA YA BUKANDWE.

KAMPUNI ya Resolute (Tanzania) Limited imetumia kiasi cha shilingi milioni 47.7 kwa ajili ya kutoa huduma za kijamii katika kata ya Bukandwe;Wilaya ya Mbogwe mkoani Geita.

Kiasi hicho kilibainishwa na Meneja wa Kampuni hiyo;William Harmworth wakati akikabidhi dawati 31 kati ya 45,katika shule ya msingi Kanegele iliyopo katika kata ya Bukandwe ikiwa ni sehemu ya miradi minne iliyopanga kuitekeleza kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Harmworth alisema mradi huo wa dawati umewagharimu kiasi cha shilingi Milioni 3.2 ambapo wanataraji kuukamilisha kwa kukabidhi dawati zingine 14 ifikapo mwishoni mwa mwezi huu.

“Tunathamini swala la elimu ndio maana tumeweka kipaumbele ufadhili kukamilisha miradi mbalimbali ya elimu na jamii ituunge mkono kwa faida ya nchi ya Tanzania”alisema Harmworth.

Alisema awali kampuni yake ilitekeleza mradi wa kisima cha pampu ya mkono kilichopo maeneo ya shule ya msingi Kanegele kilichogharimu shilingi Milioni 28.2ambapo mradi huo ulikamilika oktoba 30 mwaka jana.

Aliendelea kusema miradi mingine ambayo imeshakamilika chini ya ufadhili wa kampuni yake ni kuezeka na kukamilisha vyumba viwili vya madarasa na ofisi ya Mwalimu sambamba na kukarabati chumba kimoja cha darasa ambapo vyote viligharimu kiasi cha shilingi milioni 15.8.

Hata hivyo Meneja huyo aliiomba jamii ya kata hiyo kuibua miradi ya maendeleo na kuisimamia kwa uadilifu na kampuni yake haitosita kuwaunga mkono pindi watakapohitaji msaada wao.

Nae Diwani wa Kata ya Bukandwe;Luteni mstaafu Henly Malishi aliwakumbusha wenyeviti wa vitongoji  kuwahimiza wananchi wao kuhakikisha wanatimiza kwa wakati ahadi yao ya kuchangia madawati ili kuwanusuru vijana wao kutosoma wakiwa wamekaa chini.

Kampuni ya Resolute (Tanzania)Limited inafanya utafiti wa madini ya dhahabu tangu mwaka 2003 katika kata ya Bukandwe,Nyakafuru na Nyakasaluma za Wialya Mbogwe mkoani Geita.


0 comments: