HARAMBEE YA KATA YA BUSOKA YAFANAA.
| Mh James Lembeli mbunge wa kahama akiongoz aharambee ya kuchangia nyumba ya mwalimu na shule ya sekondari ya Busoka iliyopo kata ya |Busoka wilayani Kahama mkoa wa Shinyanga. |
Usemi
wa Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere wa “Ili maendeleo yawepo
kunahitajika Watu, Ardhi, Siasa Safi na Uongozi Bora”;
leo umerejewa kwenye Kijiji Cha Kitwana Kata ya Busoka wilayani Kahama mkoani
Shinyanga.
Tafakari
hiyo imefanywa na mbunge wa Jimbo la Kahama James Lembeli, kufuatia malalamiko
ya wananchi wa kijiji hicho kutelekezwa na uongozi wa kata hiyo katika shughuli
za maendeleo na kubaki wakimtegemea Lembeli peke yake.
Katika
mkutano huo wa Harambee ya ujenzi wa nyumba ya mwalimu wa shule ya sekondari,
wananchi wamehoji kutokuwepo kwa Diwani Mabubu Mussa, huku afisa Mtendaji wa kata
hiyo Antoni Kosta akiwa hana maandalizi yoyote.
Lembeli
amelazimika kumpigia simu Mabubu akimwomba ataje mchango wake naye akataja
shilingi 100,000=; huku Kosta akiaidi kutoa 80,000=, kiasi ambacho wananchi
walikikataa huku viongozi hao wakisusia na kudai hawana uwezo wa kutoa zaidi ya
hapo.
Katika
Mkutano huo ambao Kwa mjibu wa Lembeli,
umevunja rekodi kwa wingi wa mahudhurio, wananchi wamesema hawana imani
na uongozi wa kata ya Busoka na kwamba wangependa kujitegemea au kurudi kata ya
zamani ya Malunga.
Lembeli
amewaomba wananchi wa Kitwana bila kujali kama wametelekezwa, wajitolee
kuchangia maendeleo yao na kwamba atakuwa nao bege kwa bega, kama alivyoanza
kuchangia shilingi 2,000,000 za ujenzi wa msingi wa shule hiyo miaka mitatu
iliyopita.
Amesema
alichokiona yeye wananchi wako tayari, ardhi na siasa safi vipo,
kinachokosekana kwao ni uongozi bora na kwamba imewapasa kuchagua kamati ya
watu wanne wa kusimamia suala zima la ujenzi wa nyumba hiyo.
Wajumbe
waliochaguliwa kwenye mkutano huo ni Andrea Juma, Shija Maganga, Lameki Bupamba
na Christina Maganga wote wanatoka vijiji vya Sunge na Kitwana, huku Lembeli
akimtaja Afisa Elimu ya Msingi- Taaluma Mwalimu Amani Sabasaba kuratibu ujenzi
huo.
Katika
harambee hiyo jumla ya Shilingi 6,072,050= zikiwemo shilingi 200,000
alizochangia Mwalimu Saba, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji shilingi 600,000=,
Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo 400,000= huku Lembeli akichangia
shilingi 2,000,000= na mabati ya kuezekea.
Ziara
ya Lembeli kwa awamu hii imehusisha zaidi ya vijiji 20 Jimboni mwake, na leo
imehitimishwa katika kijiji cha Kitwana, tayari kwa kwenda kuhudhuria vikao vya
Bunge mjini Dodoma, hadi hapo atakapotoa ratiba nyingine.
MATUKIO KATIKA PICHA
| MH LEMBELI AKIWA KATIKA MSONGAMANO MKUBWA WAKATI WAKIMLAKI LEO KATIKA HARAMBEE YA SHULE YA SEKONDARI YA KATA YA BUSOKA. |
| MH LEMBELI AKIWA NA WASWEZI WACHEZAJI WA NGOMA ZA ASILI |
| MKURUGENZI MSAIDIZI WA HALMASHAURI YA MJI WA KAHAMA AKITOA MCHANGO WAKE NA M/KITI WA HALSHAURI. |
| HUYO MWENYE SHATI LA LIGHT-BLUE NDO MTENDAJI WA KATA AMBAYE WANANCHI WA KATA YAKE WAMEUKATAA MCHANGO WAKE PAMOJA NA DIWANI AMBAYE HAKUWEPO KATIKA HARAMBEE. |
| MH LEMBELI AKICHEZA NGONA NA WASWEZI. |
0 comments: