AJALI YATOKEA KITULI,SHINYANGA

    
GARI LILILOPATA AJALI ENEO AL KITULI



                                  

Watu watano wamefariki dunia na wengine wanne wamejeruhiwa katika ajali ya gari iliyotokea leo  katika eneo la kituli barabara ya  tinde,isaka mkoani shinyanga.
Kamanda wa polisi mkoa wa shinyanga evarist Mangala amekiri kutokea kwa ajali hiyo iliyohusisha toyota hiace yenye namba za usajili T 920 CDM.
 
 KAMANDA Mangala amewataja waliofariki katika ajali hiyo kuwa ni peter mwigulu(27),ambaye ni mtendaji wa kijjii cha mwantini,Jackson Moses (21),Marco methew (21)Frijinia edward(23) na mwanaume anaekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 24-25 ambae jina lake halikufahamika.

amewataja majeruhi katika ajali hiyo kuwa ni pamoja na john daud mkazi wa nyasubi kahama,stumai shaban mkazi wa chato,Charles mpenda mkazi wa nyabukande na masumbuko matias mkazi wa kakola.

Hata hivyo amesema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi na kuwa dereva wa gari hilo amekimbia na uchunguzi bado unaendelea.

Kamanda Evarist amewaonya madereva wa magari ya abiria kuwa makini wawapo barabarani kwani ajali nyingi zimekuwa zikitokea kutokana na kutokuwa makini barabarani na mwendo kasi.

T920 CDM gari iliyopata ajali inavyonekana kwa nyuma.

Damu zikiwa zimejaa ndani ya gari hilo.


0 comments: