EWURA yapandisha bei ya umeme, kuwagusa zaidi watumiaji wa majumbani...!!
Mamlaka ya Udhibiti wa huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza rasmi ongezeko la gharama
za umeme, zitakazoanza kutumika rasmi January Mosi,2014. Ongezeko hilo
limewagusa zaidi watumiaji wa majumbani wanaotumia chini ya unit 75 kwa
mwezi.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Slaam jana (December 23),
Mkurugunzi Mdhibiti Uchumi wa EWURA, Felix Ngamlagosi alisema baada ya
kupitia maombi yaliyopelekwa kwa mamlaka hiyo na Shirika la Umeme
Tanzania (Tanesco) October 1, mwaka huu, yaliyopendekeza ongezeko la bei
kwa asilimia 67, mamlaka hiyo ilipitia sababu za Tanesco na maoni ya
wadau na hivyo imeamua kupandisha bei ya nishati hiyo.
Amesema
kuanzia mwezi ujao, wateja wadogo wa majumbani hasa vijijini ambao
matumizi yao hayazidi unit 75 kwa mwezi, gharama zimeapanda kwa shilingi
40 kutoka shilingi 60 za sasa hadi shilingi 100 kwa unit moja.
Watumiaji
wakubwa wa umeme majumbani, biashara ndogo ndogo, wenye mashine za
kukoboa na kusaga nafaka, taa za barabarani, mabango, umeme umepanda kwa
shilingi 85 kutoka shilingi 221 za sasa hadi 306 kwa unit moja, sawa na
ongezeko la asilimia 40.
0 comments: