MWANAMKE NAYE AUWAWA NA WANANCHI KWA KUIBA MAHINDI MKOANI GEITA...!!


Mtu mmoja Mwanamke aitwaye Savina Sambila anayekadiriwa kuwa na miaka 20-22 mkazi wa Kitongoji cha Ilolangulo Wilayani Geita, mkoani Geita, amepigwa hadi kufa na hatimaye kuchomwa moto na wananchi kwa tuhuma za wizi wa mahindi.
Mwili wa Savina Sambila akiwa amekokewa moto na wananchi wenye hasira kali baada ya kumuua


Tukio hilo limetokea majira saa nane usiku wa kuamkia leo baada ya Sambila kukutwa akiiba Mahindi katika shamba la Milika Migeka lililopo pembeni ya nyumba yake kijini humo.
Akielezea tukio hilo
Migeka amesema alisikia mtu akivunja mahindi wakati akiwa amelala na ndipo alipotoka nje na kumkuta Marehemu Sambila akiendelea kufanya wizi huo kabla ya kumuamsha mumewe walieshirikiana kuita majirani na kumkamata.


Mwenyekiti wa kitongoji cha Ilolangulo Bw. Abel kideshe (kulia) na makamu wake Deus Lutubija  wakitoa magogo kwenye mwili wa marehemu.

Imeelezwa kuwa baada ya kumkamata Sambila walimtaka kupiga yowe na aliposhindwa ndipo walipoanza kumpiga hadi kupoteza maisha papohapo, na kisha kumchoma moto kabla ya viongozi wa kitongoji hicho kufika na kuuzima.
Mwenyekiti wa kitongoji hicho Abeli Kideshe amewataka wananchi kutokujichukulia sheria mkoni pindi panapotokea matukio kama hayo, bali wawapeleke watuhumiwa kwenye vyombo vya sheria ili haki iweze kutendeka.



Kiroba cha mahindi aliyokuwa ameiba marehemu Sabina Sambila

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Geita Kamishina msaidizi mwandamizi wa polisi Leonard Paul amethibitisa kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa uchunguzi unaendelea ili kuwabaini waliohusika na kitendo hicho ili sheria ichukue mkondo wake.
Tukio hilo limekuja siku chache tu baada ya watu watano kuwawa na kuchomwa moto katika kitogoji cha Nyantorotoro A wilayani humo baada ya kuiba rambirambi kiasi cha shilingi 65,000.
Taarifa na Valence Robert - Geita


0 comments: