MASIKINI..!! WALE MAPACHA WALIOTENGANISHWA, MMOJA UTUMBO WAKE UPO NJE
Mama
wa watoto mapacha Eliud na Elikana, Grace Joel akiwa amempakata mtoto
Eliud ambaye kwa sasa anasumbulia na tatizo la kutokwa na utumbo. Picha
na Godfrey Kahango
Suala la matibabu ya mtoto mmoja kati ya pacha waliotenganishwa
nchini India baada ya kuzaliwa wakiwa wameungana, limechukua sura mpya
baada ya mganga mkuu wa Wilaya ya Kyela, Festo Dugange kusema hajawahi
kusikia wala kumwona mtoto aliyetoka utumbo kukataliwa kutibiwa
hospitalini kwake.
Dugange alitoa kauli hiyo kutokana na wazazi wa watoto hao kuiambia
Mwananchi kwamba mtoto Eliud anaumwa na utumbo wake upo nje na kwamba
alifika Hospitali ya Wilaya ya Kyela lakini hakupatiwa matibabu kwani
daktari alimweleza kwamba anatakiwa asubiri kwenda India tu.
Mtoto Eliud na mwenzake Elikana walizaliwa Februari 20,2013 wilayani
Kyela wakiwa wameungana maeneo ya kiunoni hali iliyoilazimu Serikali
kuwapeleka nchini India ambako walitenganishwa na madaktari bingwa kwa
njia ya upasuaji.
Walirejea nchini na kufikia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Hata hivyo siku chache baada ya watoto hao kurejea kijijini kwao
Kasumulu maarufu kwa jina la Juakali wilayani Kyela, hali ya Eliud
iliaanza kubadilika baada ya sehemu kubwa ya utumbo wake mpana kutokeza
nje ya mwili.
Utumbo wa mtoto huyo umetoka nje kupitia tundu lililoachwa na madaktari jirani na kitovu chake kwa ajili ya kutolea haja kubwa.
Mwananchi ilishuhudia mtoto huyo akiwa katika hali mbaya na wazazi wa
watoto hao, Grace Daud na Erick Mwakyusa walisema walimpeleka Hospitali
ya Wilaya ya Kyela lakini walielezwa kwamba wasubiri kwenda India
walikowafanyia upasuaji ili wakarekebishe.
Mwakyusa alisema hivi sasa wanaishi naye kwa kudra za Mwenyezi Mungu na kwamba wanasubiri suala hilo la kwenda India tu.

0 comments: