Bad News_ALIYEKUWA MHADHIRI MWANDAMIZI WA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM (UDSM-SJMC) DR KAPOLI AMEFARIKI DUNIA

Dr. Irenius Kapoli enzi za uhai wake

Habari zilizoufikia mtandao huu wa malunde1 blog zinasema kuwa aliyekuwa mhadhiri mwandamizi katika chuo kikuu cha Dar es salaam(Shule Kuu ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano ya Umma-SJMC) Dr Ireneus Kapoli amefariki dunia leo (Jumamosi)alfajiri.

Chanzo chetu cha habari kimeiambia malunde1 blog kuwa Dr Kapoli amefariki dunia 
katika hospitali ya Tumbi
 huko Kibaha kutokana na BP na Kisukari. 

 Alikimbizwa hospitalini baada ya kuugua ghafla.  

Taarifa zinasema kuwa msiba uko nyumbani kwake Mbezi (Malamba mawili) jijini Dar es salaam na mazishi yanatarajia kufanyika kesho kutwa 
siku ya Jumatatu hapo nyumbani kwake.

Dr Kapoli alikuwa mtaalam wa lugha ya Kiingereza na alifanya PHD yake nchini Uingereza ,alianza kufundisha Main Campus Mlimani baadaye kuajiriwa katika Shule Kuu ya Uandishi wa habari na Mawasiliano ya Umma(sjmc).


 Alifundisha kwa muda wa zaidi ya miaka 10 hapo UDSM-SJMC,akiwa katika idara ya Lugha na  alistaafu rasmi mwaka jana.

Mbali na kufundisha smjc Dr Kapoli aliwahi kufanya kazi maeneo mbalimbali hapa nchini.

Kozi alizopata kuzifundisha katika chuo hicho enzi za uhai wake ni "Communications Skills( English for Journalists/Media),"Critical Discourse Analysis" na "Critical Thinking and Argumentation"

Dr Kapoli alikuwa mtanashati,mpenda haki,mshauri mzuri,
mwalimu bora, mwenye msimamo hakupenda upumbavu hata kidogo,,hakika aliyefundishwa na mwalimu huyu atakumbuka mengi mema ya Dr Kapoli.


Hata mkurugenzi wa blog hii ya Malunde1 ndugu Kadama Malunde alifundishwa na Dr Kapoli wakati akiwa mwanafunzi katika chuo hicho mwaka 2008/2011.

0 comments: