PICHA ZA MAJERAHA ALIYOYAPATA DIDA BAADA YA KUPOKEA KICHAPO CHA MBWA MWIZI KUTOKA KWA MUMEWE
Majeraha katika mwili wa Dida baada ya kipigo kutoka kwa mumewe Ezden.
Picha zinazoonyesha jinsi mtangazaji wa
kituo cha Redio cha Times, Khadija Shaibu alivyochezea kichapo kutoka
kwa mumewe, Edzen Jumanne zimevuja.
Picha hizo zinamuonesha Dida akiwa na majeraha makubwa sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwemo mkononi, kichwani na mapajani.
Akizungumzia kipigo hicho hivi karibuni, Dida alidai kuwa, baada ya
kutofautiana kufuatia wivu wa kimapenzi, mume wake huyo baada ya
kumporomoshea mitusi, alichukua mkanda wa suruali na kumpiga nao hadi
kumsababishia majeraha hayo hali inayomfanya muda mwingi avae kininja
kuficha aibu.
Mpaka sasa wawili hao kila mmoja kivyake huku ndoa ikielezwa kuwa haipo tena.

0 comments: